Tuesday 28 June 2016

Ziwa Natron


Ziwa Natron ni ziwa la chumvi lililopo kaskazini mwa Tanzania, karibu na mpaka wa Kenya, katika tawi la Afrika mashariki la Bonde la Ufa. Ziwa hili hulishwa na mto Ewaso Ng'iro na pia mito chemichemi zilizo tajiri kwa madini ambazo ni kina kabisa. Ziwa hili lina ukina wa chini ya mita tatu (fiti 10), na upana wake hutofautiana kwani hutegemea kiwango chake cha maji. Tofauti ya viwango vya maji kutokana na mabadiliko ya viwango vya uvukizi, ambavyo huacha viwango juu vya chumvi na madini mengine. Sehemu hii imezungukwa na eneo kavu na viwango vya mvua huyumbayumba. Mafukuto katika ziwa hili zaweza kufikia digrii 50 (celcius) au digrii 120 (Fahrenheit), na kutegemea mvua, alkalinity yaweza kufikia pH ya 9-10.5 (karibu kama vile alkali ya amonia).

 

Wanyama

Joto ya juu (hadi digrii 41 °C) na maudhui ya chumvi nyingi inayogeuka katika ziwa hili haifanyi mkono wanyamapori wengi. Hata hivyo ni makazi muhimu kwa aina ya ndege ya flamingo na pia ni makazi ya mwani, wanyama bila mifupa ya migongo na hata samaki ambao wanaweza kuishi katika maji ya chumvi. Hili ndilo ziwa pekee katika eneo la Afrika Mashariki ambalo kwa kawaida flamingo milioni 2.5 ambayo ni wadogo na ambayo huhofia maisha yao hufugwa . Kiwango ya chumvi kiongezekapo,cyanobacteria pia huongekeka, na ziwa yaweza kusaidia viota zaidi. Flamingo hawa, kundi kubwa zaidi katika Afrika Mashariki, hukusanyika pamoja katika maziwa ya chumvi, ambapo wao kujilisha Spirulina (mwani ya rangi ya buluu na kijani na pigmenti nyekundu). Ziwa Natron ni sehemu salama kufuga Flamingo wale wadogo kwa sababu mazingira yake ni kikwazo dhidi ya wanyama wanaokula wenzao wanaojaribu kufikia viota vyao. Flamingo wakuupia hufuga katika sehemu zenye ardhi zilizonyooka. Hata la kushangaza zaidi kuliko uwezo wa flamingo kuishi katika mazingira hayo ni kwamba spishi ya samaki, Tilapia wa alkali (Oreochromis alcalicus), hunawiri katika maji ya mito chemichemi.
 
 

Mimea

Rangi ya ziwa hili ni tabia ya maziwa ambayo hupata viwango vya juu sana vya uvukizi. Maji inapovukiza wakati wa kiangazi, viwango vya chumvi huongezeka na kwa uhakika, vijinyama vipendao chumvi huanza kustawi. Baadhi ya vijinyama hivi nicyanobacteria, bakteria wadogo ambao hukua majini na hujitengenezea chakula kama mimea kupitia Usanisinuru (photosynthesis) . Pigmenti nyekundu ndani ya cyanobacteria hutoa kwa kirefu rangi nyekundu ya wazi wa maji ya ziwa, na rangi ya chungwa kwa sehemu kina ya ziwa. Chumvi ya alkali ambayo hukusanyika juu ya usawa wa ziwa, mara nyingi huwa na rangi nyekundu au pinki ambayo husababishwa na vijinyama vinavyopenda chumvi na ambavyo vinaishi huko. Vinamishi vya chumvi na sehemu zenye maji bichi karibu na pembe za ziwa kufanya mkono aina tofauti ya mimea.

 

(Chanzo: Wikipedia)
 




Picha zote hapo juu zinaonyesha ziwa Natron katika hali ya kawaida
 
 
Ziwa Natron wakati wa ukame
 
 
 
 
 

No comments: